Mon, 7 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Albert Chalamila, ametoa ufafanuzi kuhusu idadi halisi ya abiria waliokuwa ndani ya ndege, waliookolewa na waliofariki dunia.
Amesema ndani ya ndege, kulikuwa na watu 43 ambapo kati yao, 24 waliokolewa na wengine 19 kufariki dunia ambapo watu wawili waliozidi kwenye idadi ya waliookolewa, hawakuwa ndani ya ndege.
Amesema mmoja kati ya waliookolewa, ni kijana shujaa aliyewaokoa watu 26, Majaliwa Jackson na mwingine ni mfanyakazi wa uwanja wa ndege, hivyo kufanya jumla ya waliookolewa kuwa 26.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live