Tue, 27 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson amesema kuwa wabunge 19 wa viti maalum wanaendelea kuwa bungeni kwa sababu wamepinga kuvuliwa uanachama na CHADEMA.
Amesema wabunge hao wamefungua kesi wakipinga kuvuliwa uanachama kwa sababu wanaona hawakutendewa haki, na kwamba kesi hii haiwezi kulinganishwa na kesi nyingine za jinai na ndio sababu wenyewe hawajafungwa.
"Ni kesi ya kisiasa, ni kesi ya uchaguzi, ni kesi ya katiba inayohusu chama chao," amesema Dkt. Tulia.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live