Dodoma. Watu 29 wamejeruhiwa katika ajali iliyohusisha lori na treni jijini Dodoma.
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Protas Katambi amesema leo asubuhi Jumanne Juni 18, 2019 kuwa ajali hiyo imetokea jana saa 5.30 usiku.
Amesema ametoa maagizo kadhaa ikiwemo kumsaka dereva wa lori ambaye inasemekana aliruka kutoka kwenye lori baada ya ajali hiyo.
Shughuli ya kuondoa mabehewa ya treni inaendelea.
Mwananchi lililopo eneo la ajali, limeshuhudia ulinzi ukiwa umeimarishwa katika eneo la tukio huku polisi waliokuwa na silaha wakiwa wameimarisha ulinzi katika tukio.
Pia, kulikuwa na abiria waliokuwa wakitoka na kuingia ndani ya treni hiyo.
Pia Soma
- Mbunge Chadema ataka kampuni ya Sicpa kuchunguzwa
- Wanawake washikana ‘uchawi’ kwenye chaguzi
- Rais Magufuli amtengua Mwenyekiti Bodi ya REA
"Bahati nzuri na Kamanda wa Polisi (Mkoa wa Dodoma- Gilles Muroto alikuwa hapa kwenye eneo la tukio ) kwa hiyo tuliagiza abiria wapewe ulinzi wa mali zao," amesema Katambi.
Endelea kufuatilia Mwananchi