Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tembo wazagaa mitaani Same, waua mmoja na kujeruhi

65423 Pic+tembozz

Thu, 4 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Moshi. Mtu mmoja amefariki dunia na mwingine kujeruhiwa, baada ya  kuvamiwa na Tembo, wakati akiwa shambani akilinda mazao yake yasiharibiwe na wanyama hao.

Kwa zaidi ya siku tano sasa makundi ya Tembo yamevamia wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro Tanzania ambapo mbali na madhara kwa binadamu, pia wameharibu  nyumba na mazao.

Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro Hamis Issah akizungumza na Mwananchi leo Julai 3,2019 amesema tukio hilo lilitokea juzi Jumatatu Julai mosi, 2019 mchana ambapo tembo hao walisababisha kifo cha Hansi  Edes (47) Mkazi wa Mheza kata ya Maole

Issah amesema tukio hilo lilitokea wakati mwananchi huyo akiwa shambani akichunga mazao yake  yasishambuliwe na tembo ambapo kundi la wanyama hao lilimvamia na kumjeruhi kichwani hali ambayo ilisababisha kifo chake.

"Wanyama  hao wametapakaa maeneo mengi ndani ya wilaya hiyo huku wakiwamo tembo wawili wakiwa wanazunguka mji wa Same. Tembo hao wawili wamezua kizazaa ndani ya wilaya hiyo na kwa sasa askari wa wanyamapori wa hifadhi ya mkomazi wanajaribu kuwarudisha ndani ya hifadhi."

Kamanda amesema mtu mmoja mwanamama ambaye amemjeruhiwa na Tembo hao, jina lake halikufahamika na kwamba alikutana na masahibu hayo, wakati akikata majani ya ng'ombe.

Pia Soma

Mmoja wa wananchi wilaya ya Same, Samoni Mjema amesema  Tembo hao wamesababisha wananchi kulazimika kujifungia ndani kuanzia saa kumi na mbili jioni kwa kuhofia kujeruhiwa na Tembo ambao wamekuwa wakizagaa ndani ya wilaya hiyo.

Chanzo: mwananchi.co.tz