Askari Polisi ambaye jina lake halikufahamika kirahisi amejikuta akihaha kujaribu kuokoa maisha ya vijana wawili maarufu 'Tatu Mzuka" wanaotumia pikipiki 'Bodaboda' zisizo na usajili kufanya matukio ya uhalifu baada ya leo kujikuta katika mikono ya raia wenye hasira kali.
Mashuhuda wa tukio hilo wameiambia 'Daily News Digital' kuwa vijana hao walionekana tangu jana wakifanya doria ya kutenda uhalifu na kwamba leo walipojaribu kumuibia mtembea kwa miguu wananchi waliwazingira na kuanza kuwaadhibu.
Tukio hilo limetokea katika eneo la Uzunguni ambapo raia wenye hasira waliamua kujichukulia sheria mkonono baada ya kushuhudia vijana hao wakivutana na mtembea kwa miguu.