Dar es Salaam. Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), umetekeleza agizo la Rais John Magufuli aliyewataka kuhama katika jengo walilopanga na kuhamia jengo la Serikali.
Oktoba 6, 2019 Rais Magufuli wakati akizindua barabara ya Tunduma- Sumbawanga yenye urefu wa kilomita 223.1, alitoa siku tano kwa Tanroads kutoka katika jengo binafsi.
Ofisi za Tanroads jijini Dar es Salaam zipo katika jengo la Airtel Morocco wilayani Kinondoni.
Soma zaidi: Magufuli atoa siku tano Tanroads kuhamisha ofisi zao, zingine mwezi mmoja
Jana Alhamisi Oktoba 10, 2019 Mwananchi lilifika katika ofisi hizo na kukuta pilikapilika za hapa na pale za baadhi ya wafanyakazi wa wakipishana kufunga mizigo.
Tanroads walipanga ghorofa ya tatu na nne, walikutwa wakihamisha vitu siku ya nne kati ya tano zilizotolewa na Rais Magufuli.
Pia Soma
- Erick Kabendera kuanza majadiliano na DPP
- Profesa Mseru: Nyerere ndio muasisi bima afya ya jamii
- Magufuli azindua barabara Katavi
Soma zaidi: Magufuli atoa siku tano Tanroads kuhamisha ofisi zao, zingine mwezi mmoja
Baadhi ya wafanyakazi wa taasisi hiyo hawakuwa tayari kuzungumza lolote wakidai kuwa sio wasemaji, lakini walisikika wakisema mchakato ulianza muda mchache baada ya agizo la Rais Magufuli.
“Kwa hali inavyokwenda kesho tunaweza kumaliza mchakato wa kuhamisha vitu ambavyo vinapelekwa kwenye ofisi mpya zilizopo karibu na ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere,” alisikika mmoja wa mfanyakazi.
Soma zaidi: Magufuli atoa siku tano Tanroads kuhamisha ofisi zao, zingine mwezi mmoja
Mfanyakazi mwingine alisikika akisema “Hali ndio kama unavyoiona hapa watu wanahamisha vitu, ofisi ile ya Mfugale (Patrick- Mtendaji mkuu wa Tanroads) watu wanaingia na kutoka. Siku za kawaida ni nadra kufanya vile.”