Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tanesco kukarabati njia ya umeme kituo cha Hale

66991 Tanesco+pic

Tue, 16 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Tanga. Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) linatarajia kufanya ukarabati wa njia ya nishati hiyo kutoka kituo cha Hale kuelekea Wilaya nne za mkoani Tanga.

Lengo la ukarabati huo ni kumaliza tatizo la umeme kukatika mara kwa mara.

Ukarabati huo ni kubadilisha nyaya chakavu na nguzo 940 zilizooza kutoka Hale kwenda Wilaya ya Muheza, Korogwe, Handeni na Kilindi pamoja na kukata miti.

Kauli hiyo imetolewa leo Jumanne Julai 16, 2019 na meneja wa Tanesco Mkoa wa Tanga, Julius Sabu akibainisha kuwa mradi huo utagharimu Sh1.2 bilioni na utatekelezwa kuanzia Julai hadi Septemba, 2019.

“Siyo kwamba muda wote wa ukarabati umeme utakatika, kuna wakati tutalazimika kuukata ili mafundi waweze kufanya kazi bila kikwazo,” amesema.

Mkuu wa Wilaya Handeni, Godwin Gondwe amesema taarifa hizo ni njema kwa wananchi wa kwa sababu ukatikaji wa mara kwa mara wa nishati hiyo umekuwa ukilalamikiwa kwa muda mrefu.

Pia Soma

Tanesco pia imetumia Sh2.6 bilioni kuunganisha umeme katika mitaa 42 ya Tanga, Muheza na Korogwe.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz