Arusha. Chama cha Wanunuzi na Wauzaji wa Madini Tanzania (Tamida) na wachimbaji wadogo wa madini ya vito Mkoa wa Arusha na Manyara wameipongeza Bajeti ya Serikali ya mwaka 2019/20 kwa kuondoa kodi za mashine za kukata madini
Akizungumza na Mwananchi, Mwenyekiti wa Tamida, Sammy Mollel amesema bajeti ya mwaka 2019/20 imeondoa kilio cha wachimbaji wa madini na wauzaji wa madini nchini.
Mollel alisema kuondolewa kwa kodi za mashine za kukata na kusanifu madini, kutaongeza ajira kwa vijana wengi, lakini pia kutaongeza mapato ya serikali kwani madini mengi yatasanifiwa nchini.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Tanzanite One na Tanzanite Forever, Faisal Juma amesema uamuzi wa Serikali kuondoa kodi katika mashine za kukata madini ni faraja kwa sekta ya madini.
“Kuondoa kodi katika mashine za kukata madini, inamaana Watanzania wengi wataanzisha viwanda vidogo vya kusanifu madini,”amesema.
Juma pia aliipongeza bajeti hiyo kwa kuanzisha kitendo cha kusikiliza malalamiko ya wafanyabiashara wanapokuwa na malalamiko ya kodi kwani sasa kutaongeza uwazi na uwajibikaji.
Habari zinazohusiana na hii
- Soma hotuba ya Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango akiwasilisha bungeni mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2019/20
- Bajeti yapanua fursa sekta ya kilimo
- VIDEO: Nywele bandia, leseni zazua mjadala Kilimanjaro
- Wananchi washangaa pato la kila mmoja kuongezeka kwa Sh100,000 kwa mwaka
“Kulikuwa na shida, unakadiriwa kodi hakuna sehemu ya kulalamika lakini pia hata TRA walikuwa hawawezi kushusha bila kupata muafaka sasa kutakuwa na chombo cha tatu ambacho kitamaliza migogoro,” amesema.
MWISHO.