Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Takukuru yabaini kasoro miradi ya maendeleo Ilala

65198 Pic+takukuru

Tue, 2 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Ilala, Tanzania umefanya ukaguzi wa miradi ya maendeleo yenye thamani ya Sh38 bilioni na kubaini upungufu katika utoaji wa malipo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Julai 2, 2019 Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Ilala, Christopher Myava amesema katika kipindi cha Aprili hadi Juni 2019 walifanya ukaguzi na uchunguzi wa tuhumiwa mbalimbali.

"Lengo la kufuatilia miradi ya maendeleo ni kuangalia thamani halisi ya fedha za umma kwenye ujenzi wa miradi ili kudhibiti uvujaji wa fedha za umma kwenye miradi ya maendeleo," amesema Myava

Amesema katika ufuatiliaji wa miradi miwili iliyoko katika sekta ya ujenzi wa barabara zilizoko maeneo yasiyopimwa katika kata ya kiwalani, ilibainika kulikuwa na upungufu katika utoaji wa malipo.

"Baadhi ya kazi za uwekaji wa zege la lami, zililipwa tofauti na ilivyoidhinishwa katika mkataba ambapo ilibainika mkandarasi alilipwa takribani Sh1 bilioni zaidi ya fedha zilizotakiwa alipwe" amesema

"Kuna barabara nyingine zilionekana kuwa na urefu mfupi tofauti na ilivyokuwa kwenye mkataba."

Pia Soma

Myava amesema katika kipindi hicho pia wamefanya uchunguzi wa tuhuma mbalimbali kwa kufungua majalada ya uchunguzi 19, yanayohusu uhujumu uchumi, ukwepaji kodi, hongo, ubadhirifu wa mali ya umma na ujenzi wa miradi ya maendeleo chini ya kiwango.

Chanzo: mwananchi.co.tz