Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Takukuru wampa siku 10 mkandarasi kukamilisha mradi wa maji Dodoma

87097 Pic+takukuru Takukuru wampa siku 10 mkandarasi kukamilisha mradi wa maji Dodoma

Thu, 5 Dec 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Chemba.  Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Dodoma,  Sosthenes Kibwengo ametoa siku 10 kwa kampuni ya Juan kukamilisha mradi wa maji wa Kelema Kuu Wilaya ya Chemba.

Wakazi wa eneo hilo wanatumia maji ya bwawa ambayo si safi na salama huku wengine wakitembea umbali wa maili mbili hadi kijiji cha Kelema Balai kutafuta huduma hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano Desemba 4, 2019 baada ya kutembelea mradi huo, Kibwengo amesema awali kampuni hiyo ililazimika kununua mabomba ya Sh51 milioni kufidia gharama ya mradi huo wa Sh223 milioni.

Amesema mradi huo ulikamilika mwaka 2014 na kufanya kazi kwa wiki moja na mabomba yake kupasuka kutokana na kuzidiwa na presha ya maji kutoka katika kisima.

Amesema kampuni hiyo ilitakiwa kutumia gharama zake kununua vifaa vinavyokidhi mahitaji ya mradi huo.

“Hizi siku kumi tulizotoa kwa kampuni hiyo zinawatosha kukamilisha mradi huu ambao wametumia muda mrefu bila kuukamilisha na ukiangalia mvua zinakaribia kuanza.”

Amesema mradi huo ungekamilika kwa wakati lakini ulicheleweshwa na walioagizwa kununua vifaa kufanya udanganyifu, kuwaomba wananchi kuwa na subira kwani wataanza kutumia maji hivi karibuni .

Chanzo: mwananchi.co.tz