Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Takukuru Tabora wapokea malalamiko 53 ya rushwa

Takukuru Tabora wapokea malalamiko 53 ya rushwa

Wed, 15 Apr 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Tabora. Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Tabora imepokea taarifa 105 za malalamiko huku 53 zikiwa za rushwa.

Akizungumza leo Jumatano Aprili 15, 2020 mkuu wa Takukuru mkoani humo, Musa Chaulo amesema taarifa nyingine 52 zilihusu makosa mengine yasiyohusiana na rushwa.

Alieleza hayo wakati akitoa taarifa za utendaji wa taasisi hiyo kuanzia Januari hadi Machi 2020, kwamba taarifa  zote zinaendelea kufanyiwa kazi.

Amebainisha kuwa wamekamilisha uchunguzi wa majalada 13, kufungua kesi mpya tano na wameshinda kesi tatu.

Amezitaja kesi walizoshinda kuwa ni ya mhudumu wa afya hospitali ya rufaa ya Mkoa aliyeomba rushwa kwa ndugu wa mgonjwa ili aongezewe damu.

Nyingine ni ya ofisa wa kampuni ya udalali aliyeomba rushwa ili wasiuze nyumba ya mteja aliyekuwa anadaiwa na benki na nyingine ni ya mtu mmoja aliyeomba rushwa kwa aliyekuwa akidaiwa kumuua mkewe ili asifikishwe mahakamani.

Pia Soma

Advertisement
Amebainisha kuwa mashauri 22  bado yanaendelea mahakamani na kusisitiza wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa taasisi hiyo ili kudhibiti rushwa mkoani Tabora.

Chanzo: mwananchi.co.tz