Moshi. Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kilimanjaro imekamata bidhaa mbalimbali zilizoingia nchini kwa njia zisizo halali.
Bidhaa hizo ni tani 4.5 za majani ya chai yanayodaiwa kutumika kutengeneza pombe feki ambayo ni kali.
Nyingine ni mafuta ya kula lita 9,482, mfuko mbadala iliyo chini ya viwango tani saba, sukari tani 4.5, maziwa ya Bruckside lita 186 na vyombo vya usafiri vilivyotumika kusafirisha bidhaa hizo ambavyo ni magari manane, pikipiki 11 na baiskeli moja.
Akizungumza leo Alhamisi Februari 13, 2020 meneja msaidizi wa forodha, Edwin Iwato amesema bidhaa hizo zimekamatwa kuanzia Julai 2019 hadi sasa.
Amesema katika bidhaa hizo, yapo majani ya chai ambayo hutumika kama malighafi ya kutengeneza pombe kali inayotengenezwa kinyemela.
"Yanatumika kutengeneza pombe haramu ambapo huyatumia kutia rangi kwenye spiriti na kutengeneza hizo pombe kali za viwandani jambo ambalo ni hatari kwa afya," amesema Iwato.
Pia Soma
- Mabula azichongea halmashauri kwa Majaliwa
- Bavicha kutumia siku wa wapendanao kuhamasisha uandikishaji daftari la wapiga kura
- Watumia zebaki bila kujali athari watakazopata