Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

TAWA yatangaza mkakati kuwalinda Flamingo wa Ziwa Natron

Mon, 24 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Arusha. Mamlaka ya usimamizi wanyamapori (TAWA) imetangaza mkakati wa kuwalinda Flamingo wa eneo   la Ramsar Ziwa Natron, lililopo wilayani Ngorongoro mkoa wa Arusha kwa kutaka eneo hilo kupandishwa hadhi kutoka ardhi owevu kuwa Pori la Akiba.

Mwenyekiti wa Bodi ya TAWA Meja Jenerali Mstaafu Hamis Semfuko amesema eneo hilo la ziwa Natroni ni la kipekee duniani hivyo kuhitaji kutunzwa na kulindwa ili Flamingo waendee kuwepo.

"Lakini  ni wajibu wa TAWA  kupanga mikakati ya kuona utalii katika eneo hili unaongezeka na kuleta mapato zaidi  yatakayowanufaisha wananchi wanaozunguka eneo hili Watanzania, TAWA na Serikali kwa ujumla" amesema.

Amesema  wanataka kulipandisha hadhi eneo hilo kutoka kuwa Pori Tengefu (Game Controlled Area) kuwa Pori la Akiba (Game Reserve).

“Tunatarajia yatafanyika kwa maridhiano kati yet una Vijiji vinavyozunguka eneo hili la Ziwa Natron, ili kurahisisha mchakato huu” amesema

Kwa upande wake Kamishna wa Uhifadhi TAWA Dk. James Wakibara amesema ndege aina ya Flamingo wanaozaliana Ziwa Natron ni maarufu duniani kutokana na maisha yao kuzingatia mahitaji nyeti.

Pia Soma

“Ndani ya Ziwa Natron kuna Kemia ya maji na aina ya Tindikali ambapo Flamingo hutanga kwenye aina ya Tindikali inayofikia kiwango cha 10 kwenda juu kidogo ukiwaweka kiwango cha Nane au 18 hawata taga.

“Inategemea duniani hiyo Kemia iko wapi,katika hili Kemia ipo Ziwa Natron ndipo tunaposema lina sifa ya kipekee duniani, kwani utakwenda kila mahali lakini ukimaliza ziwa hili Flamigo watatoweka duniani,

Chanzo: mwananchi.co.tz