Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoani Ruvuma limesema linakumbana na changamoto kubwa ya kuhujumiwa kwa kuharibiwa transifoma na kuibiwa nyaya za kopa na kusababisha hasara ya zaidi ya shilingi milioni 39.
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoani Ruvuma limesema linakumbana na changamoto kubwa ya kuhujumiwa kwa kuharibiwa transifoma na kuibiwa nyaya za kopa na kusababisha hasara ya zaidi ya shilingi milioni 39. Akiongea Eng Eliseus Mhelela ambaye ni meneja wa TANESCO mkoa wa Ruvuma amesema nyaya hizo zinaibiwa kwenye transifoma na zinakwenda kuuzwa kwenye maduka na vibanda vinavyouza chuma chakavu hivyo amewaomba wananchi wa mkoa wa Ruvuma kutoa taarifa kama watamuona mtu yeyote anafanya vitendo vya kuhujumu miundombinu ya umeme.