Mikoani. Mkoa wa Dodoma upo katika hali mbaya kwa kuwa katika orodha ya mikoa mitano inayoshika mkia tangu mwaka 2016, lakini Mkoa wa Simiyu ambao mwaka jana ulishika nafasi ya 22, safari hii umetinga kumi bora.
Katika matokeo yaliyotangazwa juzi na Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), Simiyu imeshika nafasi ya nane ikiwa na wastani wa ufaulu wa asilimia 86.46.
>> Matokeo ya darasa la saba 2019 haya hapa
Nafasi ya mkoa huo kitaifa inaonyesha mwaka 2016 na 2017, Simiyu ilishika nafasi ya 14 na 16 mtawalia kabla ya kuporomoka hadi nafasi ya 22 katika matokeo ya mwaka 2018. Katibu tawala mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini anasema matokeo hayo ni mafanikio ya pamoja ya uongozi wa Serikali chini ya maelekezo na usimamizi wa mkuu wa mkoa, Anthony Mtaka.
Kutoka katika kashfa ya moja ya wilaya zake kufutiwa matokeo katika mtihani wa mwaka jana, Mkoa wa Dodoma bado haujatengemaa. Tangu mwaka 2016, umekuwa haukosekani katika orodha ya mikoa mitano ya mwisho.
Habari zinazohusiana na hii
- Wanafunzi kumi bora wavulana matokeo darasa la saba hawa hapa
- Matokeo ya darasa la saba 2019 haya hapa
- Kanda ya ziwa yatoa shule kumi bora matokeo darasa la saba
- Somo la hisabati lawatesa watahiniwa darasa la saba 2019
>> Matokeo ya darasa la saba 2019 haya hapa
Uchambuzi wa Mwananchi unaonyesha mikoa ifuatayo imekuwa ikishika katika nafasi tano za mwisho.
Mwaka 2016 kulikuwa na mikoa ya Mbeya (22), Morogoro (23), Dodoma (24), Mtwara (25) na Songwe (26). Mwaka 2017 kulikuwa na mikoa ya Mtwara (22), Songwe (23), Dodoma (24), Manyara (25) na Singida (26).
Mwaka 2018 mikoa iliyokuwamo ni Simiyu (22), Dodoma (23), Lindi (24), Kigoma (25) na Mara (26).