Mon, 7 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mmoja wa waokoaji anasema shughuli ya kuokoaji ilisitishwa baada ya waokoaji kuingiwa na hofu ndege ya shirika la Precision Air iliyoanguka kwenye Ziwa Victoria nchini Tanzania inaweza kulipuka.
William Ruta, mkazi wa Bukoba ni miongoni mwa mashuhuda waliohusika katika zoezi la uokoaji.
Maelezo ya sauti, William Ruta: "Rubani aliwasha taa wakati tunaokoa watu tukaambiwa ndege inaweza kulipuka."
AJali hiyo imesababisha vifo vya watu 19 akiwemo rubani wa ndege hiyo huku watu wengine 26 wakiokolewa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live