Dar es salaam. Shida ya maji katika Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM) itakuwa historia ifikapo Desemba 2019.
Hayo yameelezwa leo Jumamosi Septemba 21, 2019 na Waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichako wakati akikagua miradi mbalimbali ya maji inayotekelezwa katika chuo hicho.
Amesema mfumo uliopo sasa una uwezo wa kuhifadhi maji lita 45,000 tofauti na mradi wa sasa utakaokuwa na uwezo wa kuhifadhi lita 100,000.
"Kutokana na ukubwa wa chuo hiki uwezo tulionao ni mdogo kwani maji yakikatika unakuwa usumbufu kwa wanafunzi.”
"Lengo la mradi ni kusambaza maji ili kubaki na akiba, utakapokamilika tutakuwa na uwezo wa kutumia zaidi ya siku nne ikiwa yatakatika,” amesema Profesa Ndalichako.
Amebainisha kuwa mradi huo unaogharimu Sh1.8 bilioni za makusanyo ya ndani ya chuo hicho.
Pia Soma
- Polepole ataka mashine za ukaguzi Mirerani
- Ndoto ya ofisa elimu Dar matokeo darasa la saba
- Wananchi Iringa watakiwa kuchangamkia fursa za utalii