Wed, 21 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia kutoa shilingi Milioni 920 kwa ajili ya ujenzi wa shule mbili za sekondari za Namakuku na Namichinga wilayani Ruangwa mkoani Lindi, ikiwa ni.moja ya mikakati ya serikali katika koboresha sekta ya elimu nchini.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema ujenzi wa shule hizo utasaidia wanafunzi katika maeneo hayo kutotembea umbali mrefu kwenda kufuata elimu.
Majaliwa alikuwa akikagua maendeleo ya ujenzi wa zahanati ya Namakuku pamoja na taa za barabarani kwenye kata ya Chienjele wilayani Ruangwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live