Wed, 22 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu amesema, katika kipindi cha mwaka 2021 hadi 2023 mkoa huo kupitia mamlaka za maji umepokea shilingi Bilioni 358.43 kwa ajili ya kuboresha huduma za maji ndani ya mkoa huo.
Amesema miradi 50 inatekelezwa kupitia Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Mjini (MUWSA), Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) na wizara ya Maji.
"Upatikanaji wa huduma ya maji umefikia asilimia 100 kwa upande wa mijini na asilimia 84.5 vijijini."amesema Babu
Chanzo: www.tanzaniaweb.live