Wed, 7 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Serikali imeanza majaribio ya mfumo wa ufundishaji mbashara ambao mwalimu mmoja anaweza kufundisha wanafunzi zaidi ya 1,000 kwa wakati mmoja.
Mfumo huo ambao kwa sasa unafanyiwa majaribio kwa baadhi ya shule za mikoa miwili ya Pwani na Dodoma, unamwezesha mwalimu kutoka kituo kimoja kufundisha wanafunzi wengi kwa wakati mmoja wakiwa mikoa tofauti.
Utaratibu huo unaleta tafsiri ya kwamba mbali na kurahisisha utendaji kazi, pia ni njia mojawapo ya kukabiliana na uhaba wa walimu, hasa wa masomo ya sayansi shuleni.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live