Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali yapiga marufuku uhamisho holela

FB IMG 1683001501312 1080x640 Serikali yapiga marufuku uhamisho holela

Tue, 2 May 2023 Chanzo: Dar24

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martin Shigella amepiga marufuku uhamisho holela wa watumishi pasipo kuzingatia maslahi ya uhamisho, kwani utaratibu huo unavunja moyo utendaji wa watumishi wa umma.

Shigella amesema hayo wakati akizungumza na wafanyakazi katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, kwa mkoa wa Geita, na kuelekeza kuwa taratibu za uhamisho lazima zifuatwe.

Amesema, “marufuku kumhamisha mfanyakazi kama bado bajeti ya uhamisho haipo, hayo ni amelekezo ya Rais, mkijua mnahamisha wafanyakazi kadhaa wekeni kwenye bajeti zenu, labda kama ameomba mwenyewe.”

Aidha, Shigella pia ameagiza taasisi za umma na binafsi kuhakikisha wanazingatia stahiki za wafanyakazi wanapokuwa kazini kwa muda wa ziada, kwani ni matakwa ya kisheria na ni haki kwa mtumishi na kukemea tabia ya wafanyakazi kutolipwa malimbikizo yao.

Chanzo: Dar24