Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali ya Tanzania yaitimua kampuni ya Oryx Uwanja wa Ndege wa KIA

65831 Kampuni+pic

Sun, 7 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Hai. Serikali ya Tanzania imeagiza kufutwa kwa hati ya  kampuni ya mafuta ya Oryx iliyopo ndani eneo la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Imesema eneo hilo lilichukuliwa kiujanja, kwamba haiwezekani kampuni hiyo kuwa na hati katika eneo ambalo tayari lina hati.

Agizo hilo limetolewa leo Jumamosi Julai 6, 2019 na naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wa Tanzania, Atashasta Nditiye wakati akikagua maeneo yenye mgogoro katika uwanja huo.

Ameitaka kampuni ya uendeshaji wa uwanja huo ya Kadco kutekeleza agizo hilo mara moja.

"Nimeongea na watu wa Kadco kufuta hati inayomilikiwa na Oryx. Ni jambo la kushangaza kuwa na hati ndani ya eneo lenye hati, nimeshangazwa na kusikitishwa si kitu cha kawaida.”

"Hawa Oryx wana hati ya kumiliki hili eneo katikati ya uwanja wa ndege ni kitu cha ajabu sana, iweje wamiliki hati ndani ya hati nyingine. Naomba hii hati ifutwe tunawapenda wawekezaji na tunawahitaji lakini tunataka walipe kodi kama wapangaji wengine wasimiliki ardhi kijanja,” amesema Nditiye.

Pia Soma

Kaimu mkurugenzi wa uwanja huo, Martine Kinyamagoha amesema Oryx wanamiliki eneo hilo kwa miaka 66 likiwa ndani ya hati ya uwanja huo.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz