Sun, 13 Mar 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
TIMU ya Wajumbe 11 wakiongozwa na Mkemia Mkuu wa zamani Profesa Samwel Manyele imeundwa na Ofisi ya Makamu wa Rais kuchunguza uchafuzi wa mazingira katika Mto Mara uliopelekea maji kuwa meusi na samaki kufa hovyo.
Mgodi wa Dhahabu wa North Mara tayari umeshatoa taarifa yake kutohusika na utiririshaji wa zebaki katika mto huo. Serikali kupitia kwa Mkuu wa Wilaya ya Rorya mkoani Mara imepiga marufuku matumizi ya maji na shughuli zingine ikiwemo uvuvi katika mto huo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live