Siku moja baada ya kurushwa taarifa za wananchi wa Manispaa ya Lindi kushindwa kusafiri baada ya kivuko cha MV Kitunda kilichokarabatiwa kwa garama ya shilingi bilioni 1.3 kushindwa kufanya kazi, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainabu Telacky ametoa agizo la kusitishwa kwa safari za kivuko hicho mpaka pale kitakapotengenezwa.
Siku moja baada ya kurushwa taarifa za wananchi wa Manispaa ya Lindi kushindwa kusafiri baada ya kivuko cha MV Kitunda kilichokarabatiwa kwa garama ya shilingi bilioni 1.3 kushindwa kufanya kazi, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainabu Telacky ametoa agizo la kusitishwa kwa safari za kivuko hicho mpaka pale kitakapotengenezwa. Kivuko hicho kilikuwa kwenye matengenezo mwaka mmoja uliopita na siku mbili baada ya kurejea kwa ajili ya kuanza kutoa huduma, kivuko hicho kulianza kuonesha ubovu.