Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sabaya ataka maelezo kukwama kwa nyaraka za walimu

B3fe2187065cfc1f0d26424859696d1d Sabaya ataka maelezo kukwama kwa nyaraka za walimu

Wed, 13 Jan 2021 Chanzo: habarileo.co.tz

Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya ameipa siku tatu Idara ya Utumishi wilayani humo kutoa maelezo ya kina ni kitu gani kinakwamisha ndani ya miaka miwili nyaraka za walimu wastaafu kutopelekwa kwa Katibu Mkuu wa Hazina.

“Kitendo kinachofanywa na Idara ya Utumishi wilayani humu cha kutopeleka majina ya walimu wastaafu Hazina kinaichonganisha serikali na watumishi wake kwakuwa serikali isingekosa fedha za kuwalipa wastaafu hao” amesema Sabaya.

Aidha, Sabaya amesema kuwa ndani ya hizo siku tatu anataka walimu wote waandikiwe barua na utumishi kuthibitisha madeni yao na ofisi yake itakuwa mstari wa mbele kuhakikisha walimu hao wanapata haki zao.

Chanzo: habarileo.co.tz