Mon, 7 Nov 2022
Chanzo: dar24.com
Kesi ya Uhujumu uchumi inayo mkabili Lengai Ole Sabaya imeshindwa kusikilizwa leo kutokana na Sababu za Kutokuwepo kwa Hakimu Salome Mshasha wa Mahakama ya Mkazi Moshi.
Wakili wa Sabaya, Hellen Mauna amesema wameiomba mahakama kuharakishwa kwa shauri hilo kwani mteja wake, Sabaya amepimwa na kugundulika kuwa na ugonjwa wa moyo.
"Tumeomba Mahakama itupe tarehe ya karibu mno ili vitu vyote viende kwa haraka,tunapozidi kuchelewesha hali yake inazidi kudhoofika," amesema Wakili Hellen Mahuna.
Chanzo: dar24.com