Wed, 15 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Watu saba wakazi wa Mtaa wa Majengo Mapya mkoani Morogoro wamekatwa mapanga na watu wasiojulikana wanaosadikiwa kuwa ni panya road ambao wamevamia katika maeneo wanayoishi usiku wa kuamkia leo.
Inaelezwa kuwa wavamizi hao wamevamia zaidi ya nyumba tano na walikuwa wanapiga kelele za mwizi ambazo zilikuwa zikiwafanya baadhi ya wakazi kutoka ndani.
Mwenyekiti wa mtaa huo, Magreth Kigodi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live