Sun, 5 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Idadi ya watu waliofariki kwenye ajali iliyotokea wilayani Korogwe mkoani Tanga ikihusisha gari ya mizigo ‘Fuso’ na Coaster imefikia 20 baada ya majeruhi wengine wawili kufariki leo.
Ajali hiyo ilitokea jana Februari 4, 2023 wakati wanasafirisha mwili kwenda kuzikwa mkoani Kilimanjaro ambapo 18 walifariki papo hapo.
Ratiba ya mazishi kuaga 20 waliofariki ajali Korogwe
Wawili hao wamefariki mmoja akiwa anapatiwa matibabu Hospitali ya Rufaa Bombo na mwingine Muhimbili.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live