Morogoro. Raia wa Uturuki Adem Demir mfanyakazi katika kampuni ya Yapi Markez inayoshughulika na utengenezaji wa reli ya kisasa (SGR) amefariki dunia kwa kugongwa na gari la kampuni hiyo.
Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Wilbroad Mutafungwa akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Juni 3, 2019 amesema tukio hilo lilitokea jana Jumapili Juni 2, 2019 majira ya saa 5.45 usiku huko eneo la Mkambarani ndani ya kambi ya ujenzi wa SGR.
Amesema raia huyo aligongwa na gari aina ya Man TGS Tipper mali ya kampuni ya Yapi iliokuwa ikiendeshwa na dereva Andrea.
Kamanda huyo amesema chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva huyo kutokuwa mwangalifu wakati akiendesha gari hilo ambalo lilikuwa limebeba kifusi cha udongo wakati akijiandaa kushusha.
Amesema dereva wa gari hilo amekamatwa huku mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi katika hospitali ya mkoa wa Morogoro na kukabidhiwa kwa ndugu zake kwaajili ya taratibu za kusafirisha kwenda nchini Uturuki kwa ajili ya Mazishi.
Naye mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk Steven Kebwe ameagiza kambi zote zinazofanya shughuli za ujenzi usiku na mchana kuhakikisha kunakuwa na taa na ulinzi wa kutosha na usalama.
Pia Soma
- TPSF, Trademark East Africa wajazwa mamilioni ya kufadhili mikutano
- Naibu Waziri Mgumba ataka vijiji vitenge ardhi kuajiri vijana
- Waziri Mpango akiri mkanganyiko wa sheria
- Bashe amtaka Dk Mpango kuchukua hatua kwa wezi, wanaoingiza sukari
Amesema gari hilo lilimgonga sehemu ya mguu na kuanguka chini kisha kugongwa sehemu yake ya paja na kusababisha kifo.
Mkuu huyo wa mkoa ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama amesema mtumishi huyo aliyefariki hata tochi aliokuwa akitumia ilikuwa na mwanga hafifu hivyo kusababisha dereva huyo kutoona vizuri nyuma yake na hivyo kusababisha ajali hiyo.