Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Almachius Mchunguzi amesema mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la Awadh Issa Juma (20) ambaye alikuwa ni Bodaboda katika wilaya ya Korogwe amefariki Dunia baada ya kugongana uso kwa uso na Basi la Sai Baba eneo la Msambiazi.
Akithibitisha kutokea kwa Tukio hilo, Kamanda amesema Basi la Sai Baba lilikuwa likijaribu Ku"Overtake" Lori bila kuchukua Tahadhari katika eneo ambalo haliruhusiwi hali iliyopelekea kukutana na pikipiki uso kwa uso
Kamanda amesema Baada ya kutokea kwa Ajali hiyo, Wahalifu ambao ni waendesha Pikipiki walichukua Sheria mkononi na kuweza kuchoma gari hilo moto ambalo limeteketea lote kwa moto.