Arusha. Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kupata fursa kushiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika Novemba 24, 2019.
Kauli hiyo imetolewa leo Jumatatu Oktoba 14, 2019 na kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha, Jonathan Shana baada ya kutembelea vituo vya kujiandikisha wapiga kura.
Amesema polisi wameimarisha usalama kuwawezesha wananchi kujiandikisha kwa amani na utulivu.
"Nimekuta uandikishaji umedorora natoa wito kwa wananchi kutumia siku tatu zilizoongezwa ili wajiandikishe kwa wingi,” amesema.
“Tutatumia mwongozo wa uchaguzi wa Serikali za mitaa, sheria na taratibu za polisi zilizopo katika mwongozo wa jeshi wakati wote wa kampeni, kupiga kura hadi kutangazwa matokeo.”
Amesema wasimamizi wa uchaguzi kwenye halmashauri zote za wilaya mkoani humo watawasilisha miongozo, kanuni na taratibu za uchaguzi kwa wakuu wa polisi wa Wilaya .
Pia Soma
- VIDEO: Halaiki yawa kivutio kumbukumbu kifo cha mwalimu Nyerere
- Barabara ya Dar es Salaam - Arusha yafunguliwa
- Mabaki ya mwanafunzi aliyeliwa na mamba yapatikana