Ukerewe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella amewatuliza wakazi wa kisiwa cha Siza wilayani Ukerewe Mkoa wa Mwanza kulikotokea vifo vya watu wanne akiwemo ofisa rasilimali uvuvi wa wilaya hiyo, Ibrahim Njalali.
Mongella aliyeambatana na viongozi wengine wa kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa huo, alifika katika kisiwa hicho jana Julai 23, 2019 saa1:45 usiku na kuzungumza na wakazi hao.
Usiku wa kuamkia jana yalitokea mauaji hayo katika mapigano kati ya wakazi wa kisiwa hicho na maofisa wa kikosi cha kupambana na uvuvi haramu wa kanda hiyo.
Mbali na ofisa huyo, wengine waliofariki ni Damian Joseph, Malanja Malima na Chrisant Chrisant. Katika tukio hilo askari polisi na mwananchi mmoja wamejeruhiwa.
Mongella amesema tukio hilo limetia doa Mkoa huo.
"Tutahakikisha haki inatendeka ili watu waliohusika na kitendo hiki waweze kuchukuliwa hatua," amesema Mongella akiwataka wananchi hao kuwa watulivu.
Pia Soma
- UCHOKOZI WA EDO: Tunavyomsubiri kwa hamu Bashe ‘mpya’
- Huku Marekani, Uingereza kule Iran na Serikali yake
- Daktari aeleza alivyobaini majeraha mwili wa mtoto anayedaiwa kuuawa kwa kipigo