Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

RC Mongella awapongeza wananchi, wavuvi wa Ukara

Mon, 24 Sep 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Ukara. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella amewamwagia sifa wananchi, wakazi na wavuvi wa Kisiwa cha Ukara kwa kujitolea kufanya kazi ya uokoaji tangu ajali ya Kivuko cha Mv Nyerere kilipopinduka Septemba 20,2018.

Akitoa salaam za mkoa kwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, leo Septemba 23, 2018 Mongella amesema wananchi wa kisiwa hicho walioanza kazi hiyo mara kivuko kilipopinduka na  hadi timu ya mkoa ulipowasili saa 10:45 alasiri, tayari watu 40 walikuwa wameokolewa.

"Wavuvi wa Kijiji cha Bwisya na kisiwa kizima cha Ukara wamejitolea bure boti zao za uvuvi wakipeana zamu kuopoa maiti. Ni vigumu kumshukuru mtu mmoja mmoja. Lakini Serikali ya mkoa inamshukuru kila mtu kwa nafasi yake," amesema Mongella.

Chanzo: mwananchi.co.tz