Musoma. Mkuu wa mkoa wa Mara, Adam Malima amemtaka dereva wake kutofikiria thamani ya gari lililopata ajali, bali kifo cha mtoto wake aliyekuwa akiliendesha.
Pia, Malima alimwambia dereva huyo, Shida Masaba, kuwa yuko tayari hata kutumia pikipiki ya magurudumu matatu, maarufu kwa jina la Bajaj, wakati Serikali ikimtafutia gari jingine.
Mtoto wa dereva huyo, Kasobi Shida alifariki akiwa hospitalini baada ya kuumia kwenye ajali iliyotokea Agosti 4, 2019 eneo la Kigere wakati akiendesha gari hilo la Serikali.
Akizungumza katika Ibada ya mazishi ya mtoto huyo jana, Malima alisema uhai Kasobi una thamani kubwa zaidi kuliko thamani ya gari hilo la Serikali.
Alisema tangu ateuliwe kuwa mkuu wa mkoa miaka miwili iliyopita, amekuwa akiendeshwa na Masaba kwa kutumia gari hilo wakitimiza kilomita 80,000 ambazo zilikuwa na misukosuko ya ajali na mikasa tofauti.
“Shida narudia tena kukwambia, usiwazie kuhusu gari,” alisema Malima.
Habari zinazohusiana na hii
- Dereva wa RC aruhusiwa kutoka hospitalini, mwanae kuzikwa kesho
- Gari la RC Mara lapata ajali likidaiwa kuendeshwa na mtoto wa dereva wake
- Mtoto wa dereva wa RC aliyepata ajali afariki dunia
- Alichokisema dada wa aliyefariki baada ya kupata ajali na gari ya RC
Kwa habari zaidi soma gazeti la Mwananchi la leo Alhamisi Agosti 8, 2019