Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

RC Mara amwambia dereva wake aache kuwazia gari, bali kifo cha mtoto wake

70471 Rc+pic

Thu, 8 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Musoma. Mkuu wa mkoa wa Mara, Adam Malima amemtaka dereva wake kutofikiria thamani ya gari lililopata ajali, bali kifo cha mtoto wake aliyekuwa akiliendesha.

Pia, Malima alimwambia dereva huyo, Shida Masaba, kuwa yuko tayari hata kutumia pikipiki ya magurudumu matatu, maarufu kwa jina la Bajaj, wakati Serikali ikimtafutia gari jingine.

Mtoto wa dereva huyo, Kasobi Shida alifariki akiwa hospitalini baada ya kuumia kwenye ajali iliyotokea Agosti 4, 2019  eneo la Kigere wakati akiendesha gari hilo la Serikali.

Akizungumza katika Ibada ya mazishi ya mtoto huyo jana, Malima alisema uhai Kasobi una thamani kubwa zaidi kuliko thamani ya gari hilo la Serikali.

Alisema tangu ateuliwe kuwa mkuu wa mkoa miaka miwili iliyopita, amekuwa akiendeshwa na Masaba kwa kutumia gari hilo wakitimiza kilomita 80,000 ambazo zilikuwa na misukosuko ya ajali na mikasa tofauti.

“Shida narudia tena kukwambia, usiwazie kuhusu gari,” alisema Malima.

Habari zinazohusiana na hii

 

Kwa habari zaidi soma gazeti la Mwananchi la leo Alhamisi Agosti 8, 2019

Chanzo: mwananchi.co.tz