Fri, 14 May 2021
Chanzo: ippmedia.com
Kunenge amesema serikali inatambua na kuthamini mchango wa wamachinga kwenye mkoa huo, hivyo amewataka waendelee kufanya biashara zao kwa kufuata Sheria, kanuni na taratibu.
Aidha amewataka machinga wasijenge kwenye mapito ya watembea kwa miguu wala barabarani kwasababu kwa kufanya hivyo wanahatarisha usalama wao na vyombo vya moto.
Ametoa pia angalizo kwa wafanyabiashara wenye utaratibu wa kubeba mitungi ya gesi na majiko yanayowaka na kukatizanayo katikati ya watu na vyombo vya moto jambo ambalo ni hatari kwa kiusalama.
Chanzo: ippmedia.com