Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

RC Kagera awasimamisha kazi maofisa watatu kwa ubadhirifu wa Sh600milioni

12569 Watumishi+pic TanzaniaWeb

Sat, 18 Aug 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Biharamulo.  Maofisa watatu wa halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera wamesimamishwa kazi na mkuu wa Mkoa huo Brigadia Jenerali Marco Gaguti.

Amechukua uamuzi huo ili maofisa hao wapishe uchunguzi wa upotevu wa zaidi ya Sh600 milioni ambazo hazikuwakilishwa kama mapato ya halimashauri kuanzia  2016 hadi 2018.

Hayo yamebainika jana Ijumaa Agosti 17, 2018 katika kikao maalum cha Kamati ya fedha na mipango ya  halmashauri hiyo cha kujadili taarifa ya  kamati iliyoundwa na  aliyekuwa mkuu wa Mkoa huo.

Waliosimamishwa kazi ni Alexander Bashaula ambaye ni mweka hazina wa halmashauri hiyo, Salanga Mahendeka (mhasibu) na  Emanuel Maleo ambaye ni ofisa ushirika, wote wakituhumiwa  kupoteza fedha na kukiuka  viapo vya uaminifu.

Katika kikao hicho mkuu huyo wa Mkoa amesema zaidi ya Sh690 milioni  hazikuwasilishwa kama mapato ya halmashauri kuanzia Agosti 2016 hadi Mei 2018, Sh 427 milioni hazikuwasilishwa benki na wakusanya mapato.

“Baada ya uchunguzi  wa  kamati ya katibu tawala wa mkoa wa Kagera hivi karibuni ilibainika  kuwa mwenendo wa ukusanyaji wa mapato haulidhishi  na tunachukua hatua kwa wanaopoteza fedha za umma” alisema.

Ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuanza kuchunguza  ubadhilifu huo wa mali ya umma  pamoja na kufuatilia  wote kwa ajili ya kuchukuliwa hatua za kisheria.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz