Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

RC Gambo atoa onyo kwa watakaoandamana Arusha ‘Upanga haujaribiwi shingoni’

4745 Mboo TZW

Wed, 14 Mar 2018 Chanzo: bongo5.com

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo ametoa onyo kali kwa watu watakaothubutu kuandamana mkoani humo baada ya kuzagaa kwa taarifa mitandaoni kuwa tarehe 26 April kutakuwa na maandamano ya nchi nzima.

Tokeo la picha la Mrisho gambo

Mrisho Gambo

RC Gambo amesema Arusha ni mji wa kitalii hivyo asingependa kuona usalama na amani inatoweka mkoani humo na kupoteza watalii ambao wanasaidia kukuza uchumi wa nchi.

Arusha ni mkoa wa kitalii hatuwezi kuruhusu mambo yatakayoharibu uchumi na usalama wetu, kama kuna kikundi chochote kinampango kutujaribu, tunatoa tahadhari na kuwakumbusha kuwa upanga haujaribiwi shingoni,“ameeleza Mrisho Gambo kwenye taarifa yake.

Onyo la Gambo ni muendelezo wa maonyo mengine yaliyotolewa na viongozi wengine serikalini akiwemo Rais Magufuli juu ya watu watakaoandamana siku hiyo.

Soma zaidi – Rais Magufuli atoa onyo kali kwa watu wanaopanga kuandamana

 

 

 

Chanzo: bongo5.com