Arusha. Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amewataka makamanda wa polisi Mikoa ya Kanda ya Kaskazini kushirikiana kudhibiti uhalifu kwenye mipaka kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka 2019.
Ametoa agizo hilo leo Jumamosi Desemba 14, 2019 wakati katika mkutano wa makamanda wa polisi Mikoa ya Kanda ya Kaskazini kuandaa mikakati na mbinu shirikishi za kupambana na uhalifu.
Gambo amesema kumekuwa na matukio ya uhalifu mwishoni mwa mwaka, ni muhimu kushirikiana kuyathibiti.
Mkurugenzi wa Intelejensia wa polisi, Charles Mkumbo amesema ni muhimu kuongeza mshikamano kwa makamanda hao ili kukomesha uhalifu.
Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi, Edward Bukombe amesema wakati wananchi wakijiandaa kusherekea sikukuu wahalifu nao hujipanga kufanya uhalifu, “tumejipanga kukomesha vitendo hivyo kwa kuimarisha ulinzi kwenye mipaka.”