Arumeru. Mkuu wa Mkoa wa Arusha nchini Tanzania, Mrisho Gambo ameagiza kukamatwa maofisa wa idara ya fedha katika halmashauri ya Meru mkoani humo ambao walihusika na upotevu wa vitatu vitatu vya makusanyo ya fedha.
Akizungumza katika kikao maalum cha kupitia, ripoti ya mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali (CAG) cha halmashauri hiyo jana Jumatano Julai 10, 2019, Gambo alisema watumishi waliosababisha vitabu hivyo vitatu kupotea wapelekwe polisi mara moja ili kujulikana wahusika halisi wa upotevu wa vitabu hivyo.
"Kitendo hiki cha upotevu wa vitatu kinamaanisha ni wizi uliotendeka hivyo kufunga hoja hii ni wahusika kupelekwa mahakamani au vitabu hivyo viletwe na hao pia waliotajwa wapo watu wengine nyuma,” alisema Gambo
Alisema jeshi la polisi lifanye uchanguzi wao utakaopelekea kujua ukweli kuhusu upotevu huo na taarifa zitolewe ili kukomesha vitendo hivyo.
Awali, madiwani wa halmashauri hiyo wakichambua ripoti ya CAG, walisema imebaini upotevu wa vitabu vitatu vya mapato katika halmashauri ya Meru.
Akiwasilisha taarifa hiyo, mweka hazina wilaya wa halmashauri hiyo, Jolius Ndianabo katika kikao maalimu cha Baraza la madiwani kupitia hoja ya mwaka wa fedha 2017/18 alisema suala hilo ni moja ya hoja za CAG.
Pia Soma
- Lugola awataka wananchi kubadili fikra ujenzi miradi ya maendeleo
- Udanganyifu watajwa usajili laini za simu
- Magufuli atoa onyo kwa madereva Tanzania
"Wahusika wachukuliwe hatua ili kuondosha uteketeshaji wa mali za umma kwani vitabu hivyo ni uandikishwaji wa mapato ya umma," alisema
Mkurugenzi wa halmashauri ya Meru, Emanuel Mkongo alisema wamejipanga kwa kuendelea kupata hati safi na ambao wanataka kuwarudisha ny