Thu, 18 Apr 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Albert Chalamila amechukizwa na wakandarasi wanaosimamia ujenzi wa Barabara ya mwendokasi ya Gongo la mboto.
RC Chalamila ametoa kauli hiyo mapema leo April 18 2024 alipokuwa kwenye ziara yake ambapo amesema hajaridhishwa na utendaji wa kazi wa mradi huo.
"Nataka mfanye kazi ambayo mmepewa dhamana na Serkali kwa ajili ya kuwapunguzia kero Wananchi, mkiendelea na uzembe huu ninaouona nitawaweka ndani"
Chanzo: www.tanzaniaweb.live