Mon, 3 Feb 2020
Chanzo: mwananchi.co.tz
Njombe. Polisi watatu wamekufa na wengine tisa kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wamepanda kugongana na basi na kampuni ya Sharon linalofanya safari zake kati ya Njombe na Arusha.
Akizungumza leo Jumatatu Februari 3, 2020 mganga mfawidhi wa Hospitali ya Kibena-Njombe, Dk Anord Mtega Maganga amethibitisha kupokea miili ya askari polisi hao, kwamba wengine tisa ni majeruhi.
Ajali hiyo imetokea leo alfajiriĀ eneo la kituo cha Polisi cha Mkoa wa Njombe.
Endelea kufuatilia Mwananchi kwa taarifa zaidi
Chanzo: mwananchi.co.tz