Jeshi la Polisi mkoa Tanga limefanikiwa kukamata gari aina ya Toyota Ractis yenye No.T.515DXR iliyokuwa ikitumika Kuwaibia watu mbalimbali ,huku likikamta pikipiki 18 zilizokamatwa kwa makosa mbalimbali ya Jinai.
Akitoa taarifa ya kipindi cha mwezi Oktoba mwaka huu ya misako ya Operesheni iliyofanyika ya mapambano dhidi ya uhalifu na wahalifu mkoani Tanga, Kamishna msaidizi mwandamizi wa Jeshi la Polisi mkoa wa Tanga Henry Mwaibambe alisema jeshi hilo linaendelea kupambana na uhalifu na wahalifu wanaojihusisha na makosa mbalimbali uliofanyika kwa nystatin tofauti.
Aidha ailisema kuwa mnamo tarehe13 October mwaka huu majira ya saa 11:30 huko maeneo ya Bank ya CRDB iliyopo kata ya cental Tarafa ya Ngamiani Kaskazini jijini Tanga ,ilikamatwa gari NO.T.515 aina ya Toyata Ractis ilikamatwa na mtuhumiwa alikimbia ambapo mtuhumiwa hutumia maeneo kuwaibia watu mbalimbali kwa utapeli.
Kamanda Mwaibambe alisema kuwa wakati mwingine mtuhumiwa huyo huiba kutoka ndani ya Magari ya wananchi wanaofuata huduma katika banki hiyo,hivyo jeshi la polisi linaendelea kumtafuta ili afikishwe kwenye mikono ya sheria.
Katika hatua nyingine kamanda mwaibambe alisema kuwa wamefanikiwa kakamat pikipiki 18 katika misako hiyo ya operesheni ya ndani ya mwezi moja ambapo zilikamatwa kwa makosa mbalimbali ya jinai.
Aidha Mwaibambe alitaja idadi ya pikipiki hizo katika misako inauoendelea kuwani 18 ambapo kati ya hizo pipiki 3zilikamatawa kuhusiana na uwizi wa mifugo pamoja watuhumiwa 3 wilayani Muhe,a mkoani Tanga. Aid
Sambamba hayo alisema pipiki 12 zilimakamatwa kwa makosa ya unyang'anyi wa kutumia nguvu na uporaji wa simu haswa mikoba ya kinamama ambapo watuhumiwa saba wamekatwa watafikishwa mahakamani kuhusiana na tukio hilo.
Hata alisema pikipiki 3 zilikamatwa kuhusiana na makosa ya usafirishaji wa Dawa za kulevya pamoja na usafirishwaji wahamiaji haramu ambao wameingia nchini bila Kibali.
Katika tukio nyingine alisema jeshi la polisi limefanikiwa kamata silaha bandia katika mkoa wa Tanga ambapo mnamo tarehe 3 October mwaka huu majira ya saa saba mchana huko katika maeneo ya kisosora kata ya Nguvumali tarafa ya Chumbageni katika jiji la Tanga alikamatwa Huruma John akiwa na silaha( Pistal)bandia oliyokuwa kwenye bagi lake la mgongoni ambapo mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa atafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika.