Fri, 2 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kaskazini Unguja Kamishna Msaidizi wa Polisi Daniel Shila ameitaka jamii kuacha tabia ya kutumia mitandao ya kijamii kurusha picha zenye kuleta taharuki kwa Wananchi.
Amesema picha ya video iliyosambaa katika mitandao ya kijamii ikionesha watu jamii ya Wamasai wakiwashambulia walinzi wa kampuni binafsi ya ulinzi ni tukio la muda mrefu na tayari liliishachukuliwa hatua za kisheria.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live