Tue, 14 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani limeendelea na zoezi la ukaguzi wa magari makubwa ya abiria na kuwapima madereva ulevi huku likiwataka madereva kuzingatia sheria.
Akizungumza baada ya uendeshaji na usimamizi wa zoezi hilo leo Jumanne Novemba 14, 2023, Mkuu wa Oparesheni wa Usalama Barabarani nchini, ACP Nassoro Sisiwayah amesema zoezi hili ni endelevu na litadumu mpka mwaka ujao hii ni kuhakikisha ajali zinatokomezwa,operesheni hiyo lilifanyika katika stendi ya mabasi Moshi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live