Wed, 23 Jun 2021
Chanzo: www.habarileo.co.tz
JESHI la Polisi Kamanda Maalum ya Dar es Salaam limetangaza kutoa zawadi ya Shilingi milioni mbili kwa raia atakayetoa taarifa sahihi za mhalifu akiwa na silaha hasa bunduki.
Kamanda wa polisi Kanda hiyo Mrakibu Msaidizi wa Polisi, Muliro Muliro amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Kamanda Muliro amesema jeshi hilo litahakikisha siri za mtoa taarifa zinatunzwa kwa kiwango cha juu na bila kuathiri mazingira ya usalama wake.
Amesema zawadi hizo zitaanza kutolewa bila kuzungushwa ili mradi vigezo vilivyotajwa vinazingatiwa.
Chanzo: www.habarileo.co.tz