Thu, 25 Mar 2021
Chanzo: millardayo.com
NI Machi 25, 2021 ambapo mwili wa hayati Dkt John Pombe Magufuli unaagwa na Wananchi pamoja na viongozi mbalimbali huko Chato, sasa hapa nimekusogezea picha 10 ujionee viongozi wanaoingia pamoja na Wananchi.
Endelea kukaa karibu na Ayo TV & millardayo.com tutaendelea kila matukio yanayoendelea Chato muda huu
.
.PICHANI:Kulia Jenerali Venance Mabeyo. Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Tanzania akitetaka jambo na askari mwenzake katika uwanja wa Magufuli panapofanyika shughuli za kuaga mwili wa hayati Dkt Magufuli.
.Pichani:Kulia ni Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Mhe. Innocent Bashungwa akiwa na Mkuu wa mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti wakiwa katika shughuli ya kutoa heshima za mwisho kwa Hayati Dkt Magufuli Chato
.
.Pichani:Kulia Katibu Mkuu Kiongozi Dkt Bashiru akiwa na Waziri wa Nchi, Kazi, Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama.
.J Melody akiwa jukwaani akitoa burudani
.
.Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel ni miongoni mwa viongozi wa Serikali waliofika hapa katika shughuli ya kutoa heshima za mwisho kwa Hayati Dkt Magufuli Chato
.Baraka Magufuli ni miongoni mwa wasanii waliofika hapa katika shughuli ya kutoa heshima za mwisho kwa Hayati Dkt Magufuli Chato
Chanzo: millardayo.com