Ndugu hao wa familia ya Daudi Mtuwa; Susan Mtuwa na watoto wake wawili Nathan (6) na Natalia (5) pamoja na watoto wengine wawili Cris (11) na Michelle (8) wa shemeji zake Susan walifariki dunia katika shughuli hiyo iliyofanyika Jumapili Machi 21, 2021.
Gerald Mtuwa mmoja wa wanafamilia hiyo, amesema kuwa mazishi hayo yatafanyika nyumbani kwao Kimara kuanzia kuanzia saa 4 asubuhi.
“Tunatarajia kuwazika hapa nyumbani baada ya kupata kibali kwa sababu kuna eneo kubwa. Kesho miili itawasili na kulala hapa nyumbani kesho tutaizika,” amesema Mtuwa akibainisha kuwa dada wa kazi hajapatikana wanaendelea kumtafuta.