Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ndugu waanza kupewa Sh1milioni ajali ya kivuko cha Mv Nyerere

Tue, 25 Sep 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Ukerewe. Watu 137 waliopoteza ndugu katika ajali ya kivuko cha Mv Nyerere wameanza kupokea mkono wa pole wa Sh1 milioni kwa kila marehemu aliyetambuliwa na kuchukuliwa kwa mazishi.

Awali,  ndugu hao walishakabidhiwa mkono wa pole wa Sh500, 000 kwa kila mwili uliotambuliwa.

Wameanza kupokea fedha hizo kuanzia leo asubuhi Jumanne Septemba 25, 2018.

Nyongeza ya Sh1 milioni ni agizo la Rais John Magufuli alilolitoa janam akitaka  fedha zote za rambirambi zinazochangwa na mashirika, taasisi, makampuni na watu binafsi kutumika kupewa wafiwa.

Fedha hizo pia zitatumika kujenga uzio na makaburi wanakozikwa baadhi ya waliokufa kwenye ajali hiyo iliyotokea Alhamisi Septemba 20, 2018.

Soma Zaidi:

Maiti iliyozikwa kwa kukosa ndugu yatambulika Ukerewe

Chanzo: mwananchi.co.tz