Takribani wanafunzi 1,226 wa Wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa wameshindwa kufanya mitihani ya Taifa ya Darasa la Nne mwaka huu 2021,kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za utoro, mimba na ndoa za kulazimishwa.
Mitihani hiyo ilifanyika nchini kote Septemba 8-9, 2021, ambapo jumla ya watahiniwa 1,107,469 walifanya mitihani hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, Tano Mwera, amesema kuwa idadi ya wavulana waliofanya mitihani ni kubwa kuliko wasichana.
"Kwa hakika siwezi kukataa kwamba baadhi ya wasichana wadogo wanaweza kuwa wamepachikwa mimba au kuolewa kwa lazima, hii inawezekana na ni dhahiri," alieleza.
Akichambua takwimu za walioacha shule katika kila kitongoji na idadi ya wanafunzi kwenye mabano, alitaja kata za Matai (533) Kasanga (212), Mambwe Nkoswe (153) Mwazye (159) na Mwimbi (169).