Dar es Salaam. Watu wawili raia wa Afrika Kusini wamefariki dunia baada ya ndege waliyokuwa wakisafiria kuanguka katika kijiji cha Igugwa wilayani Sikonge Mkoa wa Tabora jana Jumamosi Agosti 3, 2019.
Taarifa iliyotolewa na sekta ya mawasiliano Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano inaeleza kuwa
ndege hiyo yenye usajili ZU-TAF aina ya SLG4 ilikuwa ikiruka kutoka kiwanja cha ndege cha Tabora kuelekea kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Lilongwe, Malawi.
Inaeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni hitilafi ya injini, rubani alitoa taarifa katika kituo cha kuongozea ndege jijini Dar es Salaam na mara baada ya taarifa hiyo ndege hiyo ilipoteza mawasiliano na kuanguka.
Pia Soma
- Mfuko kulinda mtikisiko bei ya mazao Tanzania mbioni kuanzishwa
- Dk Bashiru afafanua misingi mikuu mitatu ya Chama cha Mapinduzi
- VIDEO: Lukuvi amrejeshea kiwanja Brigedia Jenerali mstaafu baada ya mgogoro wa miaka 20
Miili ya watu hao, Desmond Roy Werner (rubani) na Werner Froneman (mhudumu) imehifadhiwa katika Hospitali ya Kitete, Tabora.